UNACHOHITAJI KWENYE MAPENZI

Usimfikirie mtu ambae hana mda hata kidogo wa kukufikiria wewe.. usipoteze nguvu zaidi kwa mtu ambae hata hajibu ujumbe wako kulingana na vile ulivyohitaji aseme, unapoteza hisia zako na mda wako kwa mtu ambae haoni thamani yako.

 Upendo ni kitu ambacho hakilazimishwi, Inaweza kutokea au isotokee na kama ikitokea inatokea kwenye mkonyezo wa jicho ama ishara ya vidole.

 Upendo si kitu unachoweza kuomba au kuulizia mara kwa mara ila ni kitu ambacho kinagusa uwajibikaji, kwaiyo kama mtu hawezi kurudisha upendo usimpe umuhimu kwenye maisha yako.
Usipoteze mguso wako kwa watu wasiothamini pendo lako... kwa yule ambae kuwepo kwako au kutokuwepo hakujalishi na anakuchukulia kama mtu wa kawaida tu.

 Usichukie watu ambao walikuhitaji pindi walipotaka kitu kutoka kwako maana hao ndiyo watakaokujenga kujitambuwa kwamba wewe ni wa muhimu pia.

Kwaiyo usitoe hisia zako au mda kwa mtu ambae hata hazihitaji na kama anazihitaji ni kwa MASRAHI yake na sio kujenga muunganiko wa hisia zenu.

 Usipoteze machozi yako kwa mtu ambaye hayajali kwani ameyafanya machozi yako kuwa kama kioo chake akijitazama alivyokukamata.

Kama hawakurudishii upendo kwa upendo basi ujue kuwa huo sio upendo, Upendo hautakiwi kupanga au kujadili kama watu wawili wamepangiwa kuwa pamoja hawatakiwi kulifikiria au kulifanyia kazi kwani jambo hilo huja automatic na hutokea bila ninyi kujuwa.

Hakutakuwepo na machozi au mapigano kama ukimpata mtu ambaye anahitaji FURAHA YAKO PAMOJA NA AMANI YAKO avitazame kama ushindi wake, ni upendo ndo wenye nguvu hata mtu anaweza kukosana na ndugu ama jamii kisa Mtu ampendaye HUYO ANAKUHITAJI MAISHANI MWAKE.

Hicho ndo unachohitaji ili MOYO wako upone kwahiyo nenda umtafute huyo.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAUME MWENYE MALENGO NA WEWE UTAMTAMBUA KWA HAYA

MAPENZI NA USHIRIKINA

UMUHIMU WA KUJIANDAA NA MAISHA YA NDOA