KINACHOTESA KWENYE MAPENZI

Kinachotesa kwenye MAPENZI ni MATARAJIO na MTAZAMO wa PENZI husiaka, kuacha ni ngumu lakini ukithubutu ni USHINDI, kuachwa ni hatari lakini ukiipokea hali hiyo ni TIBA ya STRESS na yote hayo yanahitajiana kulingana na vile ambavyo unapenda kuishi na FURAHA yako MWENYEWE.

 Na usijaribu kumshika mtu ambaye yeye Mwenyewe amepanga akuondoke, akitaka kuondoka mwache aende maana ukimzuia na hana mpango nawe ITAKUGHARIMU.

Je, unalijuwa donda ndugu la MAPENZI?,
Donda la mapenzi ni MAZOEA.

 Unajuwa kupenda kila mmoja anapenda vizuri tu, Lakini ili uweze kudhihilisha pendo lako la ndani ni pale unapokuwa UMEMZOEA MTU HUYO, kama hujamzoea Mpenzi wako ni ngumu sana kuumia akiondoka, wanaoumia juu ya Mapenzi ni wale ambao kwa hakika WAMEMZOEA MTU kiasi kwamba hakuna siku ilokwenda bila kukutana, kuongea na kutumiana jumbe za mahaba.

 Kwa maana hiyo ukitaka uishi salama kwenye mapenzi achana na kumzoea mtu wako, mazoea yanatesa hasa ukijitazama na kukumbuka zile nyakati ambazo Mwenza wako aliishi nawe pembezoni mwa mbavu zako ama alivyohusika kwenye Mambo yako muhimu hakika HUTAWEZA ni ngumu mno.

 Haya mapenzi bwana yalitengenezwa mahala pabaya sana, Mapenzi yangekuwa kwenye paji la uso nani angeteswa nayo?, maana ingekuwa rahisi kujuwa USALAMA wako, lakini MAPENZI YAMEJENGWA SIRINI.

Asikudanganye Mtu eti yeye Bingwa, Kila mmoja analia kwa aina ya kilio chake ambacho kinamstahili, mimi mwenyewe naliaga juu ya wifi/shemeji yenu HUU MCHEZO UNAHITAJI AKILI.

Comments

Popular posts from this blog

MWANAUME MWENYE MALENGO NA WEWE UTAMTAMBUA KWA HAYA

UMUHIMU WA KUJIANDAA NA MAISHA YA NDOA

MAPENZI NA USHIRIKINA